Mchungaji David Mwakisole: SOMO: ASILI YA BARAKA ZETU NI KATIKA KRISTO YESU: BWANA YESU ni RAFIKI yetu. Mfano:- Ukiwa na rafiki yako unakuwa unampenda na unatamani kumfurahisha mara zote, hivyo kama unatambua kuwa BWANA YESU ni RAFIKI yako unatakiwa UMFURAHISHE, Je utamfurahishaje? • Kwa kutenda sawasawa na maagizo yake kutoka kwa Watumishi wa Mungu, ukiwa unatamani kufanya mambo mazuri kwa ajili yake ndipo anafurahi na kama kunakitu kinakuzuilia ili usifanye vizuri anakiondoa na kukuacha ukiwa huru. • Tamani kufanya mambo mazuri kwa ajili YAKE ili YEYE akufurahie na kufungua yale yaliyofungwa katika maisha yako. Ukikosa kuzingatia kinachotoka katika MADHABAHU ya Mungu dunia itakupelekesha, unapofika hemani mwa BWANA (Kanisani) unatakiwa kutafakari yanayotoka katika MADHABAHU, usiwaze tofauti na NENO linalotoka katika MADHABAHU ya BWANA maana hautapokea chochote na mwisho wa siku utatoka kama ulivyoingia.

Comments