SOMO: SALA YA BWANA.
Wafilipi 4:8 ” Hatimaye, ndugu zangu, mambo yo yote yaliyo ya kweli, yo yote yaliyo ya staha, yo yote yaliyo ya haki, yo yote yaliyo safi, yo yote yenye kupendeza, yo yote yenye sifa njema; ukiwapo wema wo wote, ikiwapo sifa nzuri yo yote, yatafakarini hayo.
• YO YOTE YALIYO YA STAHA: Hakikisha unafanya mambo ya STAHA kwa ajili ya wengine, usifanye mambo kwa kujifurahisha wewe mwenyewe hakikisha unawapendeza wengine ili wamsifu Mungu wako, usiwe mbinafsibali fanya mambo kwa ajili ya wengine.
• YO YOTE YALIYO YA HAKI: Hakikisha unakuwa mwaminifu, wewe ni HAKI ya Mungu hivyo onyesha kuwa umeibeba ile HAKI ya Mungu, usiseme mambo ya kipumbavu au ambayo watu watakulaumu, fanya mambo ambayo yatafanya watu WAFIKIE TOBA sababu wewe ni MWENYE HAKI wa Mungu. Usifanye jambo kwa kuogopa watu, fanya jambo kwa kumuogopa Mungu wako tu, acha wakuone kuwa wewe unamuogopa Mungu.
Upo hapo ulipo, katika sehemu ya chini kabisa kwa sababu humuogopi Mungu bali unawahofu watu, siku utakapo amua kumuogopa Muumba wako atakutoa hapo ulipo. Kama unataka kukua na kuongezeka sana MUOGOPE MUNGU na si wanadamu.
• YO YOTE YALIYO SAFI: Kuna mambo ambayo si dhambi lakini si mambo SAFI; Mfano:- Katika kupika, unaweza ukapika hovyo hovyo na ukaweka chakula mezani, chakula kikawa hakina Ladha nzuri, hiyo siyo dhambi lakini kufanya hivyo, sio mambo safi. Ni kitu kidogo sana lakini ukikifanya kwa usahihi unamfanya Mungu afurahi. Tunaposema MAMBO SAFI inamaana gani? Usiwafanye watu wawe na maswali kwa mambo unayo yafanya.
• YO YOTE YENYE KUPENDEZA; Hakikisha UNAPENDEZA, kama unafanya mambo na ukawaruhusu watu wakafurahia hayo ni ya kupendeza, Jifunze kusema na mkeo, mumeo, watoto wako au wakwe zako kwa namna ya KUPENDEZA, fanya mambo ambayo yatasababisha wengine wafurahi.
Chochote kilicho kizuri unatakiwa kukitenda. Unapotenda sawasawa ndipo tunasema umependeza, sio kufanya vitu visivyo halisi kama kujipodoa sana bali ni kutenda sawa sawa na kile unacho fundishwa ama kuelekezwa.
Kile unacho kitenda ndicho kitakacho sababisha SIFA NJEMA ikujilie na watu watasema vizuri kuhusu wewe. Je! Wewe watu wanasema nini kukuhusu? Je! ni sifa NJEMA au MBAYA? Hakikisha una SIFA NJEMA kama unataka Mungu awe pamoja na wewe.
Hakikisha watu wanaeneza sifa njema juu yako, wacha waseme kuwa wewe ndiye unaweza kufanya hilo jambo kwa usahihi na uaminifu, wakati wowote uwe ni mtu mwenye haki.
   :- Mtumishi wa Mungu Mtume na Nabii Josephat Elias Mwingira, Mwenge Dar es Salaam, Tanzania, EFATHA MINISTRY.

Comments