MTUMISHI WA MUNGU MTUME NA NABII JOSEPHAT ELIAS MWINGIRA.
TANGAZO LA MWAKA 2018
Isaya 40:29-31 “Huwapa nguvu wazimiao, humwongezea nguvu yeye asiyekuwa na uwezo. Hata vijana watazimia na kuchoka, na wanaume vijana wataanguka; bali wao wamngojeao BWANA watapata nguvu mpya; WATAPANDA JUU KWA MBAWA KAMA TAI; watapiga mbio, wala hawatachoka; watakwenda kwa miguu, wala hawatazimia.”
Mwaka 2018 ni Mwaka wa NGUVU, hutawahi kuzimia, hutawahi kushindwa, hutawahi kuteswa, hutawahi kuwa dhaifu, hutawahi kulala kwa sababu ya maradhi. NGUVU ya Mungu kutoka Mbinguni itakujia na kukutia NGUVU na kukupa Kushinda.
Yale yote uliyoshindwa kufanya miaka iliyopita sasa utaenda kuyafanya kwa Ushindi, ingawa unaonekana ni dhaifu lakini itatoka nguvu ndani yako na kushinda kila kizuizi kilichopo mbele yako, kamwe hutashindwa tena.
Mwaka huu utakwenda kufanya uharibifu katika kambi ya ibilisi, atalia ili kutafuta usaidizi na kamwe hataweza kupata, kilio na majonzi vitatawala katika kambi yake, popote utakapotokeza kama kuna uchawi wowote kutakuwa na mpasuko na uharibifu mkubwa. Kama kuna mchawi au mganga wa kienyeji katika familia yako Mwaka huu ni Mwaka wa kuzika. Yeyote aliyekuwa anakuzuia Kung’aa kamwe hataweza tena, Mwaka huu ni MWAKA wako kwa sababu ni Mwaka wa NGUVU hivyo USHINDI ni wako.
Watu wengi watatamani kukusogelea ili wainuliwe kwa sababu wewe utakuwa Umeinuliwa, wakati wote kuanzia sasa hadi milele hutakuwa peke yako kwa sababu UTUKUFU wa Mungu utakuja katika Maisha yako ili kusababisha NGUVU kuja kwako.
Kuhangaika na Kung’ang’ania KUMEKWISHA.

Comments