USHUHUDA:
Naitwa Piensia Mapunda. Namshukuru sana Mungu kwa matendo yake makuu kwangu. Ndani ya miaka 15 niliishi mbali na mtoto wangu, na sikujua alipokuwa, kwa sababu hakukuwa na mawasiliano kati yangu na yeye.
Siku moja akanipigia simu akaniambia kuwa anahali mbaya sana, lakini hakuniambia alikuwa wapi. Baadae nilikuja kufahamu kwamba alikuwa Tanga. Namshukuru Mungu, Baba yetu Mtume na Nabii Josephat Elias Mwingira alisema mwaka huu ni mwaka wa kujibiwa maombi, nilipofika kule Tanga, nilimkuta amekuwa mvuta bangi na mlevi wala haeleweki. Nilifanikiwa kumleta Efatha na baada ya kumleta hapa amebadilika kwani amempokea Yesu.

Comments