USHUHUDA:
Naitwa Heshima John. Napenda kumshukuru Mungu kwa matendo yake ya ajabu kwangu. Ilikuwa mwaka 2016 nilivimba tumbo nikaenda kupima nikaambiwa nina ugonjwa wa Ini na HIV. Ndipo nikaja kwenye kusanyiko kuu la mwaka 2016,Baba Mtume na Nabii Josephat Elias Mwingira akawaombea wagonjwa na mimi nikiwa mmoja wao.
Baada ya kuombewa, nikakurudi katika eneo langu la kulala, nilishangaa nikaanza kulia mwenyewe, na baadae nikaanza kucheka pasipo kujua kilichokuwa kinanichekesha, kuanzia hapo tumbo langu likaanza kuuma na nilikojoa sana na kutapika. Tumbo likaisha lote na niliporudi nyumbani nikaenda kupima haukuonekana ugonjwa wowote ule. Napenda kumshukuru sana Mungu kwa matendo yake ya ajabu kwangu, Sifa na Utukufu anastahili yeye peke yake. Sina cha zaidi cha kumpa zaidi ya kumshukuru Mungu wangu.

Comments