SOMO: ROHO MTAKATIFU:
Roho Mtakatifu anapokuja kwa mtu anamfanya huyo mtu kuwa MKAMILIFU. Ukamilifu ni nini? Ni kufanya vitu kwa usahihi bila kukosea, unapoanza biashara kama una Roho Mtakatifu hiyo biashara haitakufa bali huyu Roho ataikamilisha.
Ukiwa na Roho Mtakatifu hata unapo oa au kuolewa, ndoa yako inakuwa na ukamilifu, haitakuwa na mitikisiko wala kuyumba bali inajaa ukamilifu na Upendo.
Chochote kinacho milikiwa na Mungu kinaweza kuletwa kwako kupitia Roho Mtakatifu. Siku utakapojua namna ya kuwasiliana na Roho Mtakatifu mahangaiko yako yatakoma, kwani atakufunulia mambo yaliyofichika katika ulimwengu wa Roho.
Mtumishi wa Mungu Mtume na Nabii Josephat Elias Mwingira.

Comments