MTUME NA NABII JOSEPHAT ELIAS MWINGIRA.
Nakutamkia hutakuwa kama ulivyo kuwa, kwa maana sisi tuliookoka shetani hana Nguvu kabisa juu ya maisha yetu, sasa je! ni yupi aliye adui mkubwa kwetu? Adui mkubwa wa maisha yako ni akili yako, fahamu zako na mwili wako mwenyewe, shetani ni aduni namba mbili.
Chochote unacho kihitaji katika maisha yako kinawezekana Kama unataka kuwa mtu mkuu inawezekana, kama unataka kuwa mchawi pia inawezekana, maana Mungu ni mzuri sana amesema chochote utakachoomba kwa Jina lake atakupa.
Kama unataka kuwa chombo cha Mungu basi Mungu pia atakuletea watu wake kukusaidia ili uweze kufikia hapo . Kama unataka kuwa tajiri Mungu analeta Roho wake kukusaidia ili uweze kuwa tajiri. Kama unataka kuwa maskini Mungu atakusaidia ili uweze kuufurahia huo umaskini wako, na pia atakuletea wahubiri ambao watakusaidia kabisa kufikia lengo lako.
Mungu anao uwezo wa kukupa chochote kile ambacho unakitaka je! wewe unataka nini? Ili uweze kupokea lazima akili yako na fahamu zako zikubaliane na Mungu usiwe na uadui naye.

Comments