KUSANYIKO KUU LA TISA, EFATHA MINISTRY PRECIOUS CENTER KIBAHA:
ASKOFU: CHALRES KARIUKI - KUTOKA KENYA
Kuna vitu ambacho walipaswa kumiliki Babu zako au wazazi wako lakini hawakumiliki kwa sababu walikuwa ng’ambo ya Yordani hivyo kwa kuwa wewe Mungu amekuvusha kila ambacho Mungu aliwapa babu zako au Baba yako na hawakumiliki ni cha kwako, wao hawakumiliki kwa sababu walikufa wakiwa upande wa pili wa Yordani. Mimi na wewe tunavuka ili kumiliki nchi yetu ya Ahadi. Baba zetu walifia jangwani ili sisi tuweze kumiliki nchi ya Ahadi.
Bwana Yesu aliuchukua umaskini wetu na kuupeleka msalabani na alipokuwa anasurubiwa alisema imekwisha. Pale msalabani umaskini wako ulishindwa, pale msalabani ulipata haki yako ya kumiliki , pale msalabani ulipokea afya njema na kila kitu unacho kihitaji katika maisha yako. Ibilisi ni muongo na hauelewi msalaba kwa sababu msalaba ni kwa ajili ya kuvuka, kuacha kila shida au matatizo na kuwa mzima na kumiliki.
Biblia inasema alichukua udhaifu wetu ili mimi na wewe tusishindwe, Yesu Kristo alisulubiwa kwa sababu msalabani alifuta hatia zetu, laana, alifuta kushindwa kwetu na akatupa kushinda.
Ng’ambo utakuwa mmiliki, kwa sababu kule ng’ambo si upande wa Baba yako bali ni upande wa Baba yetu wa Mbinguni ambaye Mbingu na nchi ni mali yake hivyo atakupa kumiliki.

Comments