KAA mbali na DHAMBI, ukitenda Mema, ukitenda MATAKATIFU dhambi inakaa mbali na Wewe, lakini ukitenda ya Maovu, dhambi inakunyemelea, Uharibifu unakusogelea. Mwana wa MUNGU ACHA KUWAZA MABAYA, wala USIJIWAZIE Mabaya, MUNGU Awe wa Kwanza kwa Kuwaza yale yaliyo MAZURI katika Mawazo yako.
Mithali 8:17-21 “Nawapenda wale wanipendao, Na wale wanitafutao kwa bidii wataniona. Utajiri na Heshima ziko kwangu, Naam, Utajiri udumuo, na haki pia. Matunda yangu hupita dhahabu, naam, dhahabu safi, Na faida yangu hupita fedha iliyo teule. Natembea katika njia ya haki, Katikati ya mapito ya hukumu. Niwarithishe mali wale wanipendao, Tena nipate kuzijaza hazina zao.”
HAKUNA,…. MUNGU Akikubariki leo kesho Aache kukubariki, HAKUNA…..MUNGU Akikubariki basi ndivyo itakavyokuwa INAENDELEA, lakini lazima UMPENDE, lazima UISHI MAISHA YATAKAYOMPENDEZA MUNGU, lazima UISHI Maisha MATAKATIFU, Dhambi Ikae mbali na Wewe.
- Mtumishi wa MUNGU Mtume na Nabii Josephat Elias Mwingira, EFATHA MINISTRY.

Comments