USHUHUDA Naitwa MACKDONALD MAANYA: Natoka eneo la Shalom zone ya Ebenezer, napenda kumshukuru MUNGU kwa yale aliyonitendea, ni mengi sana lakini kubwa kabisa napenda kumtukuza MUNGU kuhusu Ndoa yangu yametokea mambo Mengi na vikwazo vingi lakini nilisimama kwamba jambo hili lazima liwezekane na hatimaye tulifunga Ndoa Takatifu katika Madhabahu ya Efatha na pia Mungu ametujalia mapacha SHONE na SAMWEL. Namshukuru MUNGU kwani Mke wangu ananifanya Nang’ara, ukiona mimi Nang’ara basi ni Mke wangu. Wewe ambaye hujaoa ndoa sio yako ni ya MUNGU wala usione kuwa kufunga Ndoa ni ngumu.

Comments