MCHUNGAJI THADAYO MBAZI MSUYA. a10Uzima ni roho wa Mungu kupitia Yesu kristo yohana 1;3-5 “Hapo mwanzo kulikuwako Neno, naye Neno alikuwako kwa Mungu, naye Neno alikuwa Mungu. Huyo mwanzo alikuwako kwa Mungu. Vyote vilifanyika kwa huyo; wala pasipo yeye hakikufanyika cho chote kilichofanyika. Ndani yake ndimo ulimokuwa uzima, nao ule uzima ulikuwa nuru ya watu. Nayo nuru yang’aa gizani, wala giza halikuiweza. “ – Ndani ya neno ndimo ulipo uzima – Neno ni pumzi na neno ni roho, – Utajuaje huyu mtu anauzima 1. UPENDO ; kuna NENO ndani yake ili Mungu ajitwalie UTUKUFU na huo uzima uwe ni NURU ambao hawajaokoka lazima uwalete kwa Yesu, hata ukisema kwa lugha ya manabii kama huna upendo ni kazi bure. Kama ukiwa na chuki huwezi kusoma biblia na wala kitabu chochote cha Efatha . Yesu alijitoa ili mimi na wewe tuwe na upendo wa kweli. Mlete mtu kwa Yesu ili upendo wake ukamilike. 2. Unaposikia Neno la Mungu unapaswa kumsoma kwani yeye anapatikana kwenye Neno usiwe mvivu wa kusoma biblia huwezi kuwa na upendo lakini, ukiwa msomaji wa biblia utakuwa na sifa ya kuitwa mfalme na utakua na neema ya kumpenda mwenzako. Tunaye baba anayefichua ya sirini upendo wa Bwana lazima ujue Neno kwanza. 3. Kama huna upendo ndani ya Efatha wewe ni maiti. Unaheri wewe uliye okoka ili uende ukawapatie wengine Neema hiyo ifanyie kazi mtumishi wa Mungu. 4. Ili uweze kumpenda Yesu lazima usome neno asubuhi mchana na jioni, 5. kaa karibu na mtu anaye mpenda Mungu kaa vizuri kwa sababu upo sehemu salama. Mimi ni nani embu kubali kukaa ndani ya Efatha Tulia mbele za Bwana upate upendo wa kweli. Amina

a10

Comments