USHUHUDA!! USHUHUDA! NAITWA THERESIA ATHANAS MOSHI Natokea Kilimanjaro KDC, wiki iliyopita nilipigiwa simu na mwanangu anayeishi Dar kuwa amepitiliza siku zake za kujifungua na kwamba ameambiwa ajiandae kwa upasuaji (Operation) kwa ajili ya kujifungua maana mtoto alikuwa hajageuka. Nikamwambia asiende kwanza hospitali anisubiri nakuja, nilipofika nikaja moja kwa moja kanisani hapa Efatha Ministry Mwenge nikaonana na Mchungaji Mwakisole, nikamweleza mwanangu ameambiwa atajifungua kwa upasuaji, Mchungaji akaomba akasema atajifungua salama kwa njia ya kawaida, ila msimpeleke hospitali hadi uchungu utakapoanza. Uchungu ulipoanza tukampeleka hospitali, manesi waligomba kwa nini tumemchelewesha, maana alitakiwa kuwahi kwa ajili ya upasuaji, mimi nikamwambia mwanangu hatajifungua kwa upasuaji. Wakasema haiwezekani maana mtoto hajageuka na mtoto akiwa katika hali hii huwa tunafanya operation ili kuokoa maisha ya mama na mtoto hivyo ni lazima apasuliwe. Nikampigia Mch. Mwakisole nikamweleza, akasema niweke simu kwenye tumbo aongee na mtoto, nikaweka akaomba. Baada ya hapo hali ya mwanangu ikawa mbaya akaanza kutapika hadi, kuishiwa nguvu. Akakimbizwa chumba cha upasuaji, mimi nikatoka nje nikimshukuru Mungu. Katika hali isiyo ya kawaida mtoto akaanza kutoka haraka kwa miguu akamalizia na kichwa, hadi manesi wakashangaa na wao walikiri kuwa ni Mungu aliyefanya. Wakaniambia usiache kumshukuru Mungu kwa jambo hili. Ndio maana nipo mahali hapa kumshukuru Mungu maana alisema kupitia Mtumishi wake Mtume na Nabii Josephat E. Mwingira kuwa sio sawa kujifungua kwa operation, bali mtoto anatakiwa kutoka kupitia njia aliyoingilia. Namshukuru pia Mchungaji mwakisole kwa kuwa pamoja nami, Mungu ambariki sana. MUNGU HASHINDWI

Comments