MCHUNGAJI DAVID MWAKISOLE: SOMO: SIRI YA BARAKA ZA MUNGU WAPI ZILIPO: Kumbukumbu la torati 28:1 "takuwa utakaposikia sauti ya Bwana, Mungu wako, kwa bidii, kutunza kuyafanya maagizo yake yote nikuagizayo leo, ndipo Bwana, Mungu wako, atakapokutukuza juu ya mataifa yote ya duniani; na baraka hizi zote zitakujilia na kukupata usikiapo sauti ya Bwana, Mungu wako. Utabarikiwa mjini, utabarikiwa na mashambani" . Baraka sio kuwa na fedha peke yake kwani unaweza kuwa na fedha na bado ukawa umelaaniwa, baraka ni kuwa karibu na MUNGU ili uweze kupokea vya kwake. Asili ya baraka zote ni YESU na ili tuweze kuzipata hizo baraka ni lazima tuachane na mambo yote yanayo haribu uhusiano wetu na YESU na kutuweka mbali na MUNGU. Inawezekana ni dhambi ya uvivu, uvivu katika mambo ya MUNGU ni kikwazo kikubwa cha kupokea baraka zetu toka kwa MUNGU.

Comments