MCHUNGAJI DAVID MWAKISOLE: SOMO: SIRI YA BARAKA ZETU WAPI ZILIPO: Baraka maana yake ni kinyume cha laana, ukiambiwa umebarikiwa maana yake hujalaaniwa na ukiambiwa umelaaniwa maana yake kwako hakuna baraka. Laana imekuja baada ya mtu kumkosea MUNGU, mtu akikwambia umelaaniwa maana yake uko mbali na MUNGU na akikwambia umebarikiwa maana yake uko karibu na MUNGU. Asili ya baraka zote ni MUNGU mwenyewe, hutaweza kuziona baraka mpaka umepatana na MUNGU na ukifarakana naye tu utaanza kuona laana zikikufuata na kila unachokifanya kinaharibika.

Comments