Mchungaji David Mwakisole: SOMO: ASILI YA BARAKA ZETU NI KATIKA KRISTO YESU: Ili tuweze kuvuta BARAKA za MUNGU kwetu ni lazima tuwe na kitu cha kumpa MUNGU, tusiende mbele zake mikono mitupu, toa nguvu zako na mali zako, baraka haziji mpaka UMEFANYA KWA BIDII ndipo wale malaika waliotumwa kwako wanapopata nguvu ya kuvuka vizuizi na kukuletea BARAKA zako. Unapokuwa na AMANI ya YESU ndipo unaweza kuzalisha vitu vingi katika maisha yako. Ili shetani akuweze kitu cha kwanza anakuondolea AMANI kwa kukukumbusha yaliyopita. Ni kweli ulikuwa mwizi, mzinzi, mlevi lakini mara baada ya kuokoka YESU alisamehe yote sasa shetani asikukumbushe ya nyuma.

Comments