Somo: MLANGO: MCHUNGAJI Angelina Mdadila: Wagalatia 4:1"Lakini nasema ya kuwa mrithi, wakati wote awapo mtoto, hana tofauti na mtumwa, angawa ni bwana wa yote". Sisi tuliookoka ni warithi pamoja na BWANA na hatutakiwi kuishi tena kama watumwa bali kama warithi. Katika maisha ya mtu yeyoye ipo milango miwili, mkubwa na mdogo, katika mlango mkubwa vinapita vitu vikubwa na vingi na katika mlango mdogo vinapita vitu vichache na vidogo. Mlango mkubwa unaruhusu vitu vikubwa na vikuu kukujia, pia ukipita katika mlango huu mkubwa unakutana na watu wakuu. Ukipita katika mlango mdogo unakutana na watu wa chini na utakutana na mambo madogo.


Comments