MTUME NA NABII JOSEPHAT E. MWINGIRA SOMO: Roho wa Bwana Juu yangu. Mungu anafikiri kufanya kitu Fulani ila humtumia mtu kukamilisha kile anachofikiria. Mtendaji ni mtu sio Mungu, Mungu anaachilia Nguvu ya kumuwezesha mtu kutenda jambo hilo alilolikusudia. Ndiyo maana akakuleta wewe duniani ili uweze kutimiza jambo fulani analohitaji lifanyike duniani. Ili uweze kutekeleza jambo lolote la Kiungu unahitaji ROHO WA BWANA. Huyu anakupa nguvu ya kukuwezesha kufanya jambo hilo. TAMANI kupokea NGUVU HII.


Comments