MCHUNGAJI: MELENIA IRENGO SOMO: TABIA Tabia ni nini? Tabia ni matendo, mienendo au sifa mbalimbali za mtu zinazoambatana na matendo yake au Nafsi yake. Tabia ziko za aina mbili:- 1. Tabia nzuri: Hii ni tabia inayotoka kwa Mungu. 2. Tabia mbaya: Hii ni Tabia inayotoka kwa ibilisi. Uwe na TABIA NZURI ili watu watamani kuwa kama wewe kwa sababu tabia nzuri INAVUTA watu karibu na wewe. Mfano mzuri ni BWANA wetu YESU KRISTO alikuwa na tabia ya KUWAVUTA WATU ILI WAMJUE MUNGU. Uwe na tabia ya kuwavuta watu ili wamjue Mungu na usiwe na tabia ya kuwakimbiza watu, iwe ni kwa maneno au kwa chochote kile mahali popote utakapokuwepo. Wagalatia 5:16-24 “Basi nasema, Enendeni kwa Roho, wala hamtazitimiza kamwe tamaa za mwili. Kwa sababu mwili hutamani ukishindana na Roho, na Roho kushindana na mwili; kwa maana hizi zimepingana, hata hamwezi kufanya mnayotaka.......”


Comments