MAMA ELIAKUNDA MWINGIRA: Usiangalie mazingira uliyonayo maana ukiangalia mazingira huta toka bali inua macho yako kwa Bwana na umtazame yeye tu maana yeye ndiye msaada wako na hata kuacha kamwe. Ndani ya Kristo Yesu kuna raha, jifunze kujitamkia mazuri maana kinywa chako kinaumba usiseme hawanipendi, maana jinsi ajionavyo mtu nafsini mwake ndivyo alivyo. Je unajionaje wewe? Mnyonge, mbaya au hufai ? Mungu hata pingana na wewe. Mungu siyo Shangazi yako wala Mjomba wako Mungu ni Mungu tu na wala usimfananishe na Mwanadamu. kama Shangazi yako au Baba yako anakuchukia usimfananishe na Mungu, Mungu wetu ni Mungu wa Upendo anakuwazia mema kila iitwapo leo.

Comments