SHUHUDA Jumapili tarehe 22/2/2015

Nilikuwa na Kibao cha Marufuku kwamba Siwezi kufaulu, lakini baada ya Kuomba na Kuvunja Kibao hicho, Nimefaulu na Nimepata DIVISION ONE.
Ester David Msimbi: Napenda kumshukuru MUNGU, katika kusoma kwangu nimekuwa nikifanya vizuri lakini nilikuwa sishiki Nafasi ya Kwanza, nilikuwa namaliza Kisutu Sekondari, wakati huo nilikuwa na mambo yangu mengi ya uongozi, nilikuwa sifanyi vizuri, nilipokuwa nafanya Mitihani nilikuwa sipati zile Division zinazo takiwa. Lakini baada ya Mafundisho ya Mchungaji wangu Mama Mdadila aliposema kuna “KIBAO cha Marufuku” kimeandikwa mbele yangu kwamba Sitafaulu, akasema “TUKIVUNJE” kile kibao, na baada ya Kuomba na Kuvunja kile kibao MUNGU Aliniona na Kunisaidia, nimepata Division ONE.
Na kuna maneno magumu kutoka kwa baba yangu mzazi alinitamkia, ya kwamba nitafeli nitapata ziro - ziro lakini MUNGU alijiinua kwangu na kunipa Kibali kwa Mwaka huu wa (Mtembeo Wa MUNGU Kwa Wale Alio Waridhia) nimepata Divison One. Lakini hii yote ni kwa sababu nilikuwa najitahidi sana katika masomo yangu lakini pamoja na hayo kuna kitu kilikuwa kinanizuia kufikia Division one, kila ninapo jitahidi nafasi yangu ilikuwa inachukuliwa na mwingine lakini MUNGU wa Efatha kutokana na maombi ya Mama Mchungaji Mdadila nimefaulu, namshukuru MUNGU sana Amina


YESU YU HAI, NI YULE YULE.....
SHUHUDA: Wana wa MUNGU wakishukuru MUNGU wetu MKUU kupata Mtoto baada ya Kukaa miaka 5.
Wana wa MUNGU pichani, waliamua kuja mbele ya Wana wa MUNGU, kuja Kumshukuru MUNGU MKUU kwa Matendo Makuu waliyotendewa, walikaa miaka 5 bila kupata Mtoto, walitiwa Nguvu na Mwana Efatha aliyekuwa anakaa nao jirani, aliwaambia "Msikate tamaa, MUNGU wetu ANAWEZA, YESU WETU YU HAI, YESU NI YULE YULE, YU HAI, ATAWAPA ITAJI LENU LA MOYO", Walizidi kuendelea Kuomba Kila siku,.. SIFA NA UTUKUFU NA UKUU ni kwa MUNGU WETU BABA YETU MKUU, AMETENDA, Hakuna JAMBO GUMU KWAKE, YEYE NI MUNGU si Binadamu, ANAWEZA, YU HAI, HAKUNA LINALOMSHINDA, Hata wewe hapo TAZAMIA KICHEKO CHAKO Sasa, POKEAAAAAA....

Comments