IBADA KUU JUMAPILI TAREHE 1/2/2015 EFATHA MWENGE

Kiongozi ibada ya sifa mass choir, Anna akiongoza mass choir kumwabudu Mungu wetu Ibadani.


Mch. Betson Kikoti, Mchungaji kiongozi Efatha Ministry Kenya, alihudumu Ibada ya kwanza, hakika Mungu wetu ni Mwema.
Mch Mese Komba wa Efatha Mbauda Arusha, akihudumu katika Ibada ya Pili Efatha Mwenge Dar es salaam

  Mimi ni Mtume Ruffas Christeen kutoka Pakistani
Nilikuwa katika kufunga na kuomba kwa siku 40 kwa ajili ya kutaka kumtafuta Baba wa kiroho ndipo Mungu akanionesha Mtume wake, Mtumishi wa Mungu Mtume na Nabii Josephat Elias Mwingira, ambaye niliona habari zake kupitia mtandao wa Internet, Mungu akanimbia nije Tanzania ndipo nitakapomuona yeye (Mungu) kupitia Mtumishi wake Mtume na Nabii Josephat Elias Mwingira, sasa ninafuraha kuwa nimempata Baba ambaye ni Mtume na Nabii Josephat Elias Mwingira, na mimi sasa ni sehemu ya Huduma ya Efatha kule Pakistan
 Mtume Ruffas Christee kutoka Pakistan akisalimia kanisa hapa Efatha Mwenge, ni mtumishi aliyeona neema ya kipekee iliyopo kwa Mtume na Nabii Josephat Elias Mwingira na amekuja ili awe chini ya Huduma ya Efatha
 Pichani: Apostle Ruffas Christee na team yake wakiwa katika Ibada ya maombi, kanisani Efatha Mwenge. Jumapili hii tumekuwa na Ibada maalumu ya maombi.

Comments