Posts

Showing posts from January, 2015

IBADA KUU TAREHE 25/01/2015 EFATHA MWENGE.

Image
Mchungaji kiongozi Kanisa la Efatha Mwenge Dar es salaam akifundisha katika Ibada ya kwanza. USHUHUDA Naitwa Vicent Sungura. Mimi napenda kumshukuru Mungu kwa yale aliyonitendea, Baba alisema tukagombee nafasi mbalimbali kwenye maeneo tunayoishi nikagombea ujumbe wa serikali ya mtaa, mtaa wa mabibo, katika kura za maoni nilishinda kwa kishindo mpaka kusimama kuwa mjumbe. Pia napenda kumshukuru Mungu kuwa nilikwenda nyasa kwetu kutangaza nia ya kugombea udiwani nilipofika songea mjini nikapigiwa simu kwamba kuna kazi ya ICT Kigoma, baadaye nilipigiwa simu nikaambiwa kuna kazi nyingine Mwanza. Wakati naingia Efatha nilimuamini mtumishi wa Mungu Mtume na Nabii Josephat Elias Mwingira nikaamua kushika maneno anayotufundisha nikaazimia mambo matatu, nilisema nitakuwa mwimbaji nimuimbie Mungu, imekuwa. Pia nilisema kwa namna yeyote nitasoma Mungu ni mwema nilipata mfadhili Naibu waziri wa miundo mbinu nimesoma mpaka chuo kikuu, nikasema nitafanya kazi nitakayoichagua yenye

IBADA KUU Tarehe 18/01/2015 EFATHA MWENGE.

Image
TABIA ....Tabia zipo za aina mbili ya kwanza ni tabia nzuri ambayo inatokana na Mungu na tabia mbaya asili yake ni shetani. ....Kutoka kwenye tabia ya dhambi siyo rahisi ndiyo maana tunamwitaji Yesu ...Unapookoka umasamehewa dhambi na unatengwa na uovu ...Unaporudi katika maisha ya dhambi unajitenga na Mungu ....Wokovu unaupokea moyoni na unadhihirishwa kwa matendo yako. ....Katika kutembea na Mungu tabia yako ni lazima ifanane na tabia ya Mungu.  Mchungaji: Mwakisole . USHUHUDA Naitwa Felista Benjamini, napenda kumshukuru Mungu kwa kunipa kibali cha kujifungua bila upasaji, ilikua si rahisi lakini kwa neema yake Mungu wakati wakujifungua ulipofika niliambiwa njia haionekani japokuwa mtoto alikuwa kageuka kwa ajili ya kutoka haikuwezekana kwani njia ilikuwa haionekani. Ikabidi nipelekwe Hospitali ya Muhimbili, nilipofika daktari wa kunifanyia upasuaji hakuwepo, alikuwa kufanya upasuaji kwa mtu mwingine. Mimi sikuacha kuomba nikimsihi Mungu n ikamwambia Mungu kama M

TEAM YA TRENET TV

Image
TEAM YA TRENET TV ikiwa kazini kwa nyakati tufauti Mungu azidi kuwatia nguvu kwa kazi yao njema ya kueneza injili kupitia TV. Trenet TV ni maono ya Mpakwa mafuta wa Bwana Mtume na Nabii Josephat Elias Mwingira. TRENET TV Inapatikana katika satelite dish na kwenye king'amuzi cha TING popote Tanzania. Wewe mwenye safari ya mbinguni hii ni chanel muhimu nyumbani kwako. Mungu akubariki na kukutunza.

IBADA KUU TAREHE 11/01/2015 EFATHA MWENGE.

Image
Mch. Victor Gasper Malamla akifundisha katika ibada ya pili Efatha Mwenge Dar es salaam Efatha Mass choir wakimtumikia Mungu kwa uimbaji mkuu.  Bwana Emilot ambaye amemwamini Mtume na Nabii Josephat Elias Mwingira, na maono ya mke aliye muoa aliyapata hapa Efatha na mke wake kujifungua salama aliamua kuchora picha ya Mtumishi na leo alikuja kumpa zawadi kama shukrani.  Watumishi wa Mungu wakifuatilia mafundisho katika ibada ya leo

IBADA KUU JUMAPILI 4/1/2015

Image
Efatha Mass choir wakimsifu Mungu wetu Ibadani. Mungu awabariki sana mnabariki wengi kwa uimbaji wenu Pichani: Mchungaji Kiongozi Efatha Mwanza Victor Gasper Malamla akifundisha Neno katika Ibada ya kwanza Efatha mwenge alivyo Baba ndivyo alivyo mwana Mungu wetu ni Mungu aokoaye na afunguaye, ngugu zetu wametoa maisha yao kwa Yesu na Yesu amewatendea Muujiza wa uponyaji na kuwafungua walio na vifungo mbalimbali.

MKESHA WA MWAKA MPYA WA 2015,PRECIOUS CENTER KIBAHA

Image
Watumishi wa Mungu wakipongezana kwa kufkia mwaka mpya 2015 mwaka wa Mtembeo wa Mungu  Waziri wa maliasili na Utalii Lazaro Nyalando akitoa salamu za Mwaka mpya 2015 kwa wana Efatha hapa Precious Center Kibaha "Namshukuru sana Mungu na nimebarikiwa sana na walivyo imba waimbaji, Mungu alisema katika siku za mwisho vijana watapata maono. Mungu ameifanya efatha kuwa lango la kubarikiwa Tanzania." Nina kila sababu kucheza, Acheni nicheze, aliyoyatenda Mungu kwa wana efatha ni makubwa na anayoenda kuyatenda kwa wana Efatha mwaka huu 2015  Mama Eliakunda mwingira akiongoza maombi... Mungu wetu upewe sifa mwanaume wa wanaume upewe sifa Efatha mass choir wakimwabudu na kumsifu Mungu. Hakika ni siku ya kipekee sana hasa kwa waliopata kibali kuwepo mahali hapa