SHUHUDA IBADA ZA LEO


Mch Merania Irengo wa Eneo la Amani
Anamshukuru Mungu kwa kuchaguliwa kutenda kazi karibu na mtumishi wa Mungu Mtume na Nabii Josephat Elias Mwingira.
Pia namshukuru Mungu kwa sababu kuna siku mtu mtumishi wa Mungu alisema kila mtu ambaye watoto wao wako nchi za nje warudi nyumbani ili watumikie taifa lao, nikaingia katika maombi Mungu ni mwema mwaka jana mwanangu aliye zamia marekani alirudi nyumbani na mwingine wa kike amerudi, mmoja aliyeolewa Uganda naye karibini atakuja nyumbani na mumewe, kwa kweli namshukuru Mungu
Kwenye kusanyiko la mwaka huu 2014 Mtumishi wa Mungu alisema kuna watu wanaenda kupokea zawadi, nakumbuka tarehe 14 mwezi huu wa kumi na mbili mshirika wangu mama mmoja akanipigia simu kuuliza kama nipo nyumbani nika mwambia nipo baada ya dakika 45 alikuja akanipa gari funguo kadi ya gari na kila kitu akaniambia amenipa gari ili inisaidie katika majukumu yangu ya kichungaji. Hatimaye na mimi namiliki gari kweli Mungu amenishangaza, namshukuru sana Mungu. Nataka ujue changamoto hazina mchungaji kila mtu anachangamoto anazopita nazo lakini kama unaye Mungu atafanya njia kwa ajili yako. Pili neno kutoka kwa mtumishi wa Mungu lina nguvu ya kusababisha jambo litokee. Amen

Comments