KUKAA NDANI YA YESU

Ukikaa ndani ya Yesu kunamambo makubwa yanatokea kwako, ndio maana alitoka mbinguni akaja kukaa ndani yangu. Yesu Kristo alikuwa mbegu kwaajiri yangu kwahiyo anataka mimi na wewe tumzalie matunda. Bwana anataka na mimi na wewe tuzae watu wengi tukaandaye kanisa kwaajiri ya unyakuo.

Yohana 15:1-20 Yesu ananena na wanafunzi wake, anawaasa wanafunzi wake anawapa maagizo anasema mimi ndimi mzabibi na uzima, na kila tawi linalozaa ndani yake huzaa, lisiro zaa hukatwa. Kama wewe haupo ndani ya Yesu ni vigumu sana kuzaa matunda. Mwanzo 23:26 Yesu anasema hatutauwa tasa wala matubo yetu hayata haribika. Ili uzae ndani ya Yesu kuna kuzaa matunda, Yesu alikuwa mzabibu mwema na amenipanda ndani ya mzabibu mwema. U

Ukiona tabia yako hajawa njema basi Yesu hayupo ndani yako, kama Yesu alikuwa mtii lazima uwe mtii kiburi kinatoka wapi?. Hakuna kitu kibaya wewe umeokoka harafu siku unaenda mbinguni Mungu anasema sikujui kitu kibaya sana.

Yesu alikuja kuufanya ulimwengu umgeukie Mungu kutokana na wanadamu wamegeuka na kutenda dhambi. Umeletwa ili umzalie Mungu matuda,Yesu alipoenda kwenye ule mtini alipouangalia anataka matunda kwake alikosa aliulaani ule mti. Angalia usilaaniwe, tusababishe maongezeko katika ufalme wa Mungu, kunafaida katika kuzaa matunda. Kuzaa sio kazi, kazi nikutunza na kunyonyesha.

KUNA FAIDA TUNAPOZAA MATUNDA TENA YALE YANAO DUMU.
1.     Ukikaa ndani ya Yesu anakutendea mema
2.     Pendo la kristo linahamia kwako ukishika amri zake. Yesu akasema pendaneni, Ila sisi wapendwa hatupendani wala hatusalimiani. Je tutafika mbinguni? Usikubali kukwazika wala kuwa mrokole jina tu. Upendo huhimili yote
3.     Faida nyingine tunakuwa  rafiki wa Yesu. Fungu la 10 ni ulinzi wa kutosha
4.     Faida nyingine anakutoa kunako utumwa na anakufunulia siri zake. Ibrahimu alikuwa rafiki wa Mungu.

5.     Huwezi kuyafanya ya dunia ukiwa na urafiki na Mungu kwani  ukipendwa na Dunia ujue hujakaa ndani ya Mungu. Ulimwengu  ulimchukia Yesu lazima dunia ikuchukie ni lazima ujue wewe ni rafiki wa Mungu. Using’anganie dini. Kila mtu ataitwa kivyake umeletwa huku duniani kwa kusudi fanya mapenzi ya Mungu. Kazi ya dini inakuweka kwenye kibano ili usiweze kumjua baba yako halisi ndio baba wako wa siri, dini ni mlezi,kaa ndani ya Yesu tembea na Yule aliekuita. Mwili ulionao hauna dhamani siku Mungu akiutoa kwenye huo mwili wanakimbiza kuzika.  Fanya kazi ya kuamrisha mwili sio mwili ukuamrishe wewe. Kaa ndani ya Yesu ili ubaki kwenye mti ili uweze kupaliliwa na Mungu kama mti mzabibu. 

Comments