Posts

Showing posts from August, 2014

Wana wa MUNGU walioamua kuja kwa YESU

Image
Nendeni duniani kote mkawafanye mataifa yote kuwa wanafunzi wangu... Ni agizo la BWANA wetu YESU KRISTO kuwaleta watu kwake, kuwaleta watu kwenye NURU, kuwaleta kwenye kuwekwa HURU, lazima tutafute kilichopotea, Tutafute Kondoo, wengi bado wanateseka katika mamlaka ya nguvu za giza, wakati YESU Alikufa kwa ajili yetu, hebu timiza agizo hili mlete mtu kwa YESU ili naye aondokane na mateso anayopata, huo ndio UPENDO. Pichani: Wana wa MUNGU walioamua kuja kwa YESU, walioamua kuyakabidhi maisha yao kwa BWANA wetu YESU KRISTO, na tunamshukuru MUNGU wetu MUNGU MKUU kwa kutupa Kibali na Neema cha kuwaleta watu kwa YESU KRISTO BWANA wetu kila Ibada, kila Jumapili Efatha Ministry Mwenge, Dar es Salaam, Tanzania.

IBADA YA JUMAPILI 18/8/2014

Image
PICHA MBALIMBALI Ibada ya Leo   Zaituni Mteiya – Shaloom – sikuwahi kuonana na Baba yangu tangu 2005 pia sijaonana na mama yangu aliyeolewa Ulaya. Alipoenda ulaya hakutaka kabisa kuwasiliana na sis watoto wake aliwashirikisha watumishi kuhusu jambo hilo, siku moja Mtume na Nabii alitamka kwamba mwezi huu Mungu ataenda kuwashangaza watu. Mwaka mmoja ulio pita mama alikuwa anawasiliana na mume wangu lakini, alikuwa hatujali wanawe kwa lolote, alikuwa akiwajali na kuwanunulia ndugu zake nyumba na vitu vingine. Mungu alinishangaza baada ya mama yangu kupiga simu na kutaka kuongea na nami aliniomba nimwandalie hotel wakati sio kitu cha kawaida alipokuja mama alinipa pesa nyingi, gari aina ya URO, anamshukuru Mungu sana. Mariamu Mdosa – Shaloom : Mwanafunzi chuo cha muhimbili ninasomea mionzi namshukuru Mungu kwa hilo moja, katika chuo ninachosoma tulitakiwa kuandaa project na mimi nilikuwa sina ujuzi kuhusu kuandaa project. Lakini mwezi huu nilikuwa nimeka a na kufi

SHUHUDA IBADA YA PILI 10/8/2014

Image
Dada Emmy Natokea Gongolamboto nilikuja Dar es Salaam nikafikia kwa mama mkwe kwa ajili ya kujifungua mama mkwe akanishuhudia matendo makuu ya MUNGU yanayotendeka ndani ya Huduma ya Efatha, mama yake alinifundisha um uhimu wa matoleo ya ZAKA fungu la Kumi. siku moja nilikuja kanisani siku hiyo Baba aliwaita wajawazito na mimi nikaombewa nilijifungua salama pasipo matatizo yeyote. LEO nimekuja kumshukuru MUNGU wa Efatha.

MTUME NA NABII JOSEPHAT E. MWINGIRA

Image
MTUME NA NABII JOSEPHAT E. MWINGIRA Akiongoza Ibada katika Madhabahu ya Kitume na Kinabii Efatha Ministry Mwenge.

KONA YA EFATHA MIKOANI NA NJE YA NCHI

Image
EFATHA MINISTRY KILIMANJARO , Mchungaji wake Kiongozi ni Mch. Oscar Mgaya Mtumishi wa MUNGU Mchungaji Kiongozi Efatha Ministry Kilimanjaro, Mch. Oscar Mgaya akipita na kuwawekea mikono na kuwaombea mmoja mmoja wote Ibadani (Jumapili tarehe 3 August 2014)     Pichani: Mchungaji Kiongozi na Mama Mchungaji na Wachungaji Wasaidizi wakiwa katika Kumuimbia na Kumchezea BWANA MUNGU wetu MKUU, jana Ibadani tarehe 3 August 2014 Pichani: Hii ni Office ya Mchungaji   Pichani: Hayo ni Mazingira mazuri yanayozunguka Hema ya BWANA.   Pichani: Ni Shule ya Watoto, Efatha Ministry Kilimanjaro KDC Day Care Centre EFATHA MINISTRY RUVUMA   Pichani:  ni Ibada ya Ubatizo ukiwa unafanyika, Wana wa MUNGU wanauzika Utu wa Kale, Picha nyingine ni Ukombozi (Deliverance) ukifanyika kw a Wana wa MUNGU. Efatha Ministry Ruvuma inaongozwa na Mchungaji Kiongozi Mch. Philipo James. EFATHA MINISTRY KAGERA. Pichani:hiyo ndio ilikuwa Hema ya BWANA ya Mwanzo kabisa wakati Hu