Posts

Showing posts from September, 2013

MANENO YENYE HEKIMA NA UFAHAMU

MANENO YENYE HEKIMA NA UFAHAMU: (Mkalimani Mtumishi wa MUNGU Mtume na Nabii Josephat Elias Mwingira). ''MUNGU Anasema, “Wenye Haki wana mateso mengi”! Watu watasema, mbona huyu ana shida sana, mbona yuko hivi na hivi….waambie ni kweli maana wenye haki wana mateso mengi! Wayahudi ni watoto wake MUNGU, na MUNGU Alimwambia Ibrahim Atambariki na Watoto wake wote lakini wakawa Watumwa katika Nchi ya M isri. Wakamlilia MUNGU katika shida zao, katika maangamizo yao Wakamlilia BWANA kwa miaka 400 na BWANA AKAWAOKOA. “Usione nina mateso mengi, yupo ANAYEKUJA KUNIOKOA”! N.B. Kutoka Kanisa kwenda Kanisa, kwenda mikutano mbalimbali ya maombi HAIWEZI Kukutoa kwenye Matatizo mpaka UTAKAPOAMUA KUTOKA KWENYE TATIZO, Mpaka UTAKAPOAMUA na KUAMINI na KUKUBALI KWAMBA HAKI yako INATOKA kwa MUNGU na UNAIPATA kwa Sababu YESU KRISTO AMEKUFA KWA AJILI YAKO na AMELIPA DENI ZAKO ZOTE (Hapo ndipo UTATOKA KWENYE TATIZO). Lakini bila ya kuelewa hivyo, utazunguka Makanisa mengi na Utaombew

KUWEKWA WAKFU MBELE ZA BWANA

Image
Mtumishi wa MUNGU Mama Eliakunda Josephat Elias Mwingira, akiongea na Wana wa MUNGU kabla ya kuanza kuwaweka Wakfu wanae kwa ajili ya BWANA   Mtumishi wa MUNGU Joshua Josephat Elias Mwingira, akijibu SWALI Aliloulizwa ''KAMA YUKO TAYARI KUMTUMIKIA MUNGU BWANA WETU na BABA YETU",... Joshua ALIJIBU "YUKO TAYARI KUMTUMIKIA MUNGU WETU na BABA YETU ALIYE MKUU"       Mtumishi wa MUNGU Anna Josephat Elias Mwingira, akijibu SWALI Aliloulizwa ''KAMA YUKO TAYARI KUMTUMIKIA MUNGU BWANA WETU na BABA YETU",... Anna ALIJIBU "YUKO TAYARI KUMTUMIKIA MUNGU WETU na BABA YETU ALIYE MKUU"   Wana wa MUNGU Joshua na Anna wakiwa wamepiga magoti tayari kwa Kupakwa Mafuta kwa ajili ya UTUMISHI kwa MUNGU WETU BABA ALIYE MKUU na MMWEMA Sana.   Wana wa MUNGU wakiwa wamepiga magoti kwa Unyenyekevu tayari kwa UTUMISHI.

KUSANYIKO KUU LA BWANA 2013 LIMEKARIBIA

Image
Mtumishi wa MUNGU Natushila akionyesha Vazi la Kanga, ambalo linafaa kwa Watu wote, Wakina baba wanaweza kushona Vitenge... Ni Vazi Zuri la Kusanyiko hili la Baraka tele kwa MUNGU wetu ALIYE MKUU na MUWEZA   Haleluya,... KUSANYIKO KUU LA BWANA 2013 Limekaribia,... Kibaha Precious Centre, Tanzania. Wana wa MUNGU Tusikose Baraka hii Aliyotujalia MUNGU WETU MZURI. ''Watumishi wa MUNGU akiwapo Suzy Msofe wakionyesha Mavazi yenye NGUVU ya MUNGU WETU MKUU ya Mwaka huu 2013''

SHUHUDA SHUHUDA SHUHUDA.

Image
MUNGU Wetu na BABA Yetu ni MZURI MNO, Anatupenda sana Wanawe,... Katika YESU KRISTO Bwana na Mwokozi wetu, MUNGU WETU MKUU wa EFATHA,... Wana wa MUNGU hawa Jane na Denis Mr & Mrs, waliamua leo kuja mbele za Wana w a MUNGU, mbele ya Hema ya BWANA kuja Kushuhudia Matendo MAKUU ya MUNGU WETU na BABA YETU MKUU Aliyowatendea katika Maisha yao. Walioana miaka 5 iliyopita, Lakini katika miaka yote hiyo Hawakuweza kufanikiwa kupata Mtoto, Hospitalini waliambiwa kuwa HAWAWEZI Kupata MTOTO KAMWE, Kwani Hawana MBEGU ZA KUZALISHA Watoto,... Madaktari waliwapima na kuwapa majibu hayo kila Hospitali mbalimbali walizokwenda kutibiwa. Lakini Hawakukata tamaa,... Walimwamini MUNGU wetu MKUU, MUNGU wa EFATHA kuwa ATAWAPA Watoto,... Kwenye Kusanyiko la wana wa MUNGU la Mwaka jana 2012 Kibaha Precious Centre, Mtumishi wa MUNGU Mtume na Nabii Josephat Elias Mwingira aliita Wale wote ambao Hawajapata watoto ili Awaombee,... Huyu mwana wa MUNGU Jane alitoka mbele na kuombewa,... Haleluy

SIKU YA KUJONGEA HEMANI MWA BWANA

Kesho ni Siku ya JUMAPILI, ni Siku ya kujongea Hemani mwa BWANA MUNGU Wetu MKUU ALIYE HAI,... ni siku ya kuwa Nyumbani mwa BWANA BABA YETU MUNGU MKUU... Haleluya Tukimsikiliza Mtumishi wake Mpenzi Mkalimani wetu Mtume na Nabii Josephat Elias Mwingira akitupa Siri na Ufunuo wa BABA MUNGU WETU MKUU ANAYETUPENDA SANA Wanae,... Haleluya, BARAKA, SIFA, UTUKUFU, UKUU Ni Wake YEYE ALIYE PEKE YAKE MUNGU WETU MKUU. Amani Iwe Nanyi Katika Kujongea Mbele za BWANA MUNGU Wetu, ... Tutazame Mioyo Yetu Isije Ikatufungia YALIYOMEMA TOKA MADHABAHUNI PAKE, Haleluya... USHINDI Ni Wake MUNGU WETU MKUU, BARAKA na UTUKUFU Ni ZAKE Haleluya ... Msikose Kuja Kupokea YALIYO MEMA YA MUNGU WETU MKUU Toka Madhabahuni Pake, Haleluya.

MANENO YENYE HEKIMA NA UFAHAMU: (Mkalimani Mtumishi wa MUNGU Mtume na Nabii Josephat Elias Mwingira).

''Hebu fuatia kisa cha mmoja wa Mitume wa BWANA YESU. Yuda Iskariote, alikuwa mmoja wa mitume 12 wa awali ambao BWANA YESU aliwateua miongoni mwa wengi Waliomfuata. BWANA YESU, Alijitenga ili Aombe kwa MUNGU usiku kucha peke yake ndipo Alipofanya Uteuzi wao. Bila shaka alifanya hivyo ili apate He kima ya kuchagua watu walio sahihi. (Luka 6:12-16). Tena Yuda Iskariote, alipewa kutunza hazina ya Huduma, ikimaanisha kuwa alihakikishwa katikati ya wengi walioteuliwa. Baada ya mafunzo ya Huduma ya BWANA YESU, Mitume hawa walihitimu na kutumwa peke yao kwenda kuhudumia watu Dhidi ya mapepo wote, maradhi yote, na Kutangaza Ufalme wa MUNGU. Yuda alikuwa mmoja wao, ikimaanisha kuwa alikuwa na Sifa zilizotakiwa (Luka 9:1-6) (Inawezekana kabisa kuwa YESU Alijua fika Yuda alikuwa na MOYO MBAYA lakini Alimchagua ili ATUFUNDISHE JAMBO Fulani). BWANA YESU na Mitume walivyoendelea na Huduma, yalizuka maswali ya faida gani watapata kwa kumfuata YESU na Huduma yake, hasa kwa ku

MANENO YENYE HEKIMA NA UFAHAMU: (Mkalimani Mtumishi wa MUNGU Mtume na Nabii Josephat Elias Mwingira).

''Watu wengi wameumizwa na marafiki wa karibu kwa sababu hawakujua wanawawazia nini kila siku. Tunashuhudia Serikali zikipinduliwa na Marafiki miongoni mwa kundi hilo hilo, pia Mauaji ya halaiki yakifanywa na watu wanaofahamiana, kwa sababu Moyo wa Mwanadamu ni mdanganyifu. Siyo rahisi kufahamu a nachowaza wakati wowote. Tunasoma, “Moyo huwa mdanganyifu kuliko vitu vyote, una ugonjwa wa kufisha; Nani Awezaye kuujua?” (Yeremia 17:9). Moyo hubadilika kila wakati kutegemeana na mazingira na mazoea ya mtu aliyojijengea. Wapendanao wanaweza kufarakana vikali na chuki ya kutisha kuibuka kwa sababu ya moyo!. Mtu bila KUJIJUA, anaweza kuwa na Kijicho, Hila, Matusi, Ukorofi, Kiburi, Upumbavu n.k. mambo ambayo ni MATUNDA ya Moyo. Ndani ya moyo wa Mtu hutoka Mawazo mabaya, Uasherati, Wivu, Uuaji, Uzinzi, Husuda na Kadhalika. Maovu haya yote yanamtia mtu Unajisi, ni VIZURI KUYASHUGHULIKIA. Biblia inasema; “Akasema, kimtokacho mtu ndicho kimtiacho unajisi” (Marko 7:20 -23).

MANENO YENYE HEKIMA NA UFAHAMU: (Mkalimani Mtumishi wa MUNGU Mtume na Nabii Josephat Elias Mwingira).

ANENO YENYE HEKIMA NA UFAHAMU: (Mkalimani Mtumishi wa MUNGU Mtume na Nabii Josephat Elias Mwingira). ''Biblia inatuambia kuwa, bila kujali uwezo wako wa kusali au mahali unaposali, yako maovu yanayokushuhudia ya kuwa umepungua. Tunasoma, “Ijapokuwa maovu yetu yanatushuhudia, lakini utende wewe kwa ajili ya Jina lako, Ee BWANA! Maana kurudi nyuma kwetu ni kwingi, tumekutenda dhambi.” (Yeremia 14: 7) Maovu yetu yanatushuhudia kwa sababu moyo wetu umeiacha sheria ya MUNGU na kushika mapokeo ya wanadamu. Na hicho tulichokipokea ndicho kinachotushuhudia leo. - Mfano:- Moyo una maandalio, au kitu unachotafuta lakini mara yanapotokea matatizo mtu huyu anaweza kufuta kila kitu chema kutoka kwa MUNGU kutokana na jinsi anavyo kabiliana na changamoto hizo Imeandikwa, “Maandalio ya moyo ni ya mwanadamu, lakini jibu la ulimi hutoka kwa BWANA” (Mithali 16:1). Biblia inatufundisha kuwa wakati wana wa Israeli walipokuwa wakirudi katika nchi yao ya ahadi kutoka utumwani Misri,

UWEPO NDANI YA KANISA SEPT 1

Image
  Ni Wewe tu BABA Uliye MUNGU wetu, Hakuna Mwingine...   Ni BABA YETU TU, Asante MUNGU Wetu...   Uwepo wa MUNGU.   Asante MUNGU Wetu... Wana wa MUNGU wakifuta Machozi,.. si Machozi ya Kupigwa Hapana...     YESU BWANA Wetu, Tunakupenda..   Wana wa MUNGU wakiwa katika Roho wakiongea na MUNGU BABA Yetu,... si machozi hayo ya kufiwa au kupigwa bali ni UWEPO NDANI YA KRISTO YESU BWANA Wetu.

TUNAKUA NDANI YA KRISTO

Image
  UPENDO wa BABA MUNGU WETU kwa Wana wa MUNGU Watoto Wake...   Waacheni watoto waje kwangu, Wala MSIWAZUIE. Watoto wakiwa na Upako, NGUVU ya MUNGU wetu MKUU wakiwaombea Wana wa MUNGU Watu Wazima,... Je Wewe Mzazi, Mlezi, Upendi Mwanao Awe na Katika Upako NGUVU ya MUNGU Wetu Hii?... Kwa JINA LA YESU KRISTO wa NAZARETH,... mapepo yanakimbia, Watu wanaponywa, vifungo vinafunguka, Watu wanawekwa HURU... OOooh Jamani YESU NI MZURIII.     Waleeni watoto katika Misingi ya IMANI, nao Watakula Mema ya Nchi,...   Wazazi, Walezi... Msikose kuwa na Watoto wenu Hemani mwa BWANA,... kwani Kumcha BWANA ndio chanzo cha Maarifa... Je Hupendi mwanao awe na Maarifa ya MUNGU wetu MKUU?,... Sunday School zipo Mahali pote Efatha Ministry,... Mkuze Mwanao ndani ya KRISTO BWANA, ili HOFU YA MUNGU WETU MKUU IUMBIKE NDANI YAKE,... Naye Atakuwa katika BWANA...   Haleluya, Usikose kutenda Vema nawe Uta....  Watoto wakicheza mbele za bwana,inapendeza sana watoto kuk